Mkuki Na Nyota Publishers

UPEPO, MCHANGA, ANGA: Hadithi Tatu

Sh 12,000

Marc Eichen

SKU: 9789987753147 Categories: , , , Tag:

“Katika miaka zaidi ya 20 ya kufundisha Kiswahili kwa wageni, sijakutana na andiko la hadithi nzuri kama hizi alizoandika mwandiihi Marc Eichen. Ufundi wake wa kutumia vitushi halisi, na kuvisana kwa maumbo mbalimbali ya lugha ni wa kipekee! Hadithi tatu hizi ni mchango mkubwa katika ufundishaji wa Kiswahili na fasihi kwa wenyeji na ugenini. Zitawasaidia pakubwa walimu pamoja na wanafunzi kufahamu uhondo wa lugha za Kiswahili na Kiingereza kupitia vipengele mbalimbali vya lugha aliyotumia mwandishi.
Ndugu Suleiman Khalfan na Abdulrahman Ndegwa vilevile wametoa tafsiri ya haki, wakilenga kabisa alichodhamimiria mwandishi wa hadithi zenyewe.”
–Dkt. David Kyeu
Coordinator and Continuing Lecturer, Center for African Studies
Chuo Kikuu cha California, Berkeley

“Hadithi katika kitabu cha Upepo, Mchanga na Anga ni fupi, lakini zenye maana. Hadithi hizi zimejikita katika mandhari ya visiwa vya Zanzibar katika Afrika Mashariki, taswira hizi za wazi zinamwalika msomaji kuandamana na wahusika wanaopitia changamoto za kibinafsi ndani ya eneo linalobadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya kijamii na kiuchumi, utalii, na hata mabadiliko ya tabianchi. Kitabu hiki kitawavutia wanafunzi wa Kiswahili na Afrika Mashariki kwa ujumla, na kwa upana zaidi wale wanaotaka kuelewa mivutano ya kitamaduni na mabadiliko yanayohusiana na utandawazi.”
–Caitlyn Bolton, PhD
Chuo cha Boston

Dimensions 130 × 195 mm

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “UPEPO, MCHANGA, ANGA: Hadithi Tatu”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also like…