Mkuki Na Nyota Publishers

Diwani ya Tuzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein – 2

Author(s): Ebrahim Hussein, fasihi ya Kiswahili, Gerald Belkin, poetry prize, Swahili poetry, Tanzanian poetry, tuzo ya ushairi, ushairi

Sh 15,000

Diwani ya pili ya Tuzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein, iliyoanzishwa kutokana na wosia wa hayati Gerald Belkin kwa heshima ya Profesa Hussein. Mashairi teule ya washindi na washiriki wa shindano, pamoja na tafsiri za Kiingereza za washindi watatu wa kwanza. A bilingual anthology of the Ebrahim Hussein Poetry Prize, second edition.

Diwani ya pili ya Tuzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein, tuzo iliyoanzishwa kutokana na wosia wa hayati Gerald Belkin, muongozaji filamu aliyekuja Tanzania kutengeneza filamu kuhusu maisha ya ujamaa vijijini miaka ya 1960 na 1970. Belkin alifanya kazi bega kwa bega na Profesa Ebrahim Hussein, mwanazuoni maarufu na mwandishi wa tamthilia na mashairi, na kabla ya kufariki aliacha fedha ili kushindanisha washairi wa Tanzania kwa heshima ya mchango wa Hussein kwa fasihi ya Kiswahili. Diwani hii ina mashairi teule ya washindi na washiriki wa shindano, pamoja na tafsiri za Kiingereza za mashairi ya washindi watatu wa kwanza. Washairi ni wa mchanganyiko: vijana, wazee, wanaume na wanawake, wakiakisi hali ya Tanzania na Afrika ya leo.

Dimensions 230 × 150 mm
Binding

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Diwani ya Tuzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein – 2”

Your email address will not be published. Required fields are marked *