Diwani ya mashairi ya Kiswahili ya Mohammed Khelef Ghassani. Mateso, maumivu, na siasa ni mambo yaliyojaa uchochezi mkali unaomsukuma mshairi kuzungumza waziwazi na kinagaubaga, na hatimaye kumfanya mwandishi apandwe na jazba zinazofanya kazi fulani itoke nje ya kingo za ulingo wa kisanaa. Mshairi lazima atunge wimbo unaoimbika ndani ya nafsi yake mwenyewe kwanza, wimbo utakaomwezesha kunyanyuka kitandani asubuhi huku akijua hayuko pweke, ana wenzake wenye maumivu kama au kuliko yake. Mohammed Ghassani ana weledi huu wa kubaki ndani ya kingo za ulingo wa kisanaa, weledi wa kuichenga siasa kwa namna ya kuipa nguvu kubwa zinazoficha na kuzimua unagaubaga na ukali wake. Mwandishi alizaliwa mwaka 1977 visiwani Zanzibar na ametunga diwani kadhaa; diwani yake N’na Kwetu ilimpatia Tuzo ya Fasihi ya Kiafrika kwa Lugha ya Kiswahili ya Mabati-Cornell mwaka 2015.

Machozi Yamenishiya
Author(s): diwani, fasihi ya Kiafrika, Kiswahili, Mabati-Cornell, Mohammed Ghassani, siasa, ushairi, Zanzibar
Sh 15,000
Diwani ya mashairi ya Kiswahili ya Mohammed Khelef Ghassani, mshairi kutoka Zanzibar aliyeshinda Tuzo ya Fasihi ya Kiafrika kwa Lugha ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya 2015 kwa diwani yake N’na Kwetu. Mashairi yanayoangazia mateso, maumivu, na siasa kwa weledi wa kisanaa.
ISBN: 9789987083756
Category: Poetry
Tags: diwani, fasihi ya Kiafrika, Kiswahili, Mabati-Cornell, Mohammed Ghassani, siasa, ushairi, Zanzibar
Be the first to review “Machozi Yamenishiya”Cancel Reply
Related products
-

Moto wa Kifuu
Sh 10,000 -

Voice of Agony
Sh 40,000 -

Chemichemi Jangwani
Sh 12,000 -

Mmeza Fupa
Sh 18,000
Reviews
There are no reviews yet.