Mkuki Na Nyota Publishers

Kibanda cha Mkaa

Sh 8,000

Athumani Mauya

Kichuguu kinawavutia wapita njia nao wanakigeuza mtaji. Hamadi! palipokuwa na kuchuguu panazaa ufuska, vurugu na visa tele. Linakuwa jiji la raha na karaha zote? Mgodi wa Mbovili. Mgodi unaotema madini na kutunisha mifuko ya wengi waingiao na kuwapa kiburi kisichomithilika.

Mgoli naye hali bado kinda, ananaswa kwenye tandabui la huba la mwalimu wake, Mkebe, aliyetumia mwanya wa hali ngumu ya maisha ya Mgoli kumrubuni kwa kumpatia vijisenti vya matumizi. Huba linampeleka puta Mgoli, hata ashindwe kujinasua. Husemwa haba na haba hujaza kibaba na kinga na kinga ndipo moto uwakapo. Mgoli aliyeonja asali, anajiingiza katika penzi jingine la Babu Jimi, mfanyabiashara maarufu wa madini. Akiwa na wanaume hawa wawili, Mgoli anapata ujauzito. Haya baba wa mtoto ni nani? Na nini hatma ya Mgoli?

Kuhusu Mwandishi

Athumani Mauya ni Mwalimu mstaafu kutoka Bagamoyo. Anaishi jijini Dar es Salaam na familia yake. Riwaya yake nyingine iliyochapishwa na Mkuki na Nyota ni ‘Harusi ya Dogoli’

Dimensions 195 × 130 mm
Binding

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Kibanda cha Mkaa”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also like…