Mkuki Na Nyota Publishers

Haki, Amani na Maendeleo

Sh 9,000

S. J. Bwana

SKU: 9789987080021 Categories: , , Tag:

Haki, amani maendeleo ni vitu muhimu katika maisha ya binadamu. Binadamu hawezi kupata maendeleo ya kweli kama hakuna haki. Aidha maendeleo hayapatikani kama hakuna amani. Nayo amani haitakuwepo kama hakuna haki. Mambo yote hayo matatu yanategemeana. Pamoja na kutegemeana huko, haki inachukua nafasi ya kwanza kwani ndiyo inayozaa hayo mengine mawili. Miongoni mwa mambo mengine, kitabu hiki kinajadili mfumo wa utoaji haki nchini Tanzania, mahakama za Tanzania, hali halisi katika mahakama hizo na nini kifanyike ili kurekebisha mambo. Mwandishi wa kitabu hiki, Mh. Jaji Steven James Bwana, amekuwa mtumishi wa Mahakama tangu mwaka 1975. Alihitimu shahada ya kwanza ya sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1974. Mwaka 1977, alipata shahada ya uzamili (Kriminolojia na Penolojia) kutoka chuo hicho hicho.Baadaye alijiunga na chuo kikuu cha Lateran (Roma) na kutunukiwa shahada nyingine ya uzamili (Civil Law). Mnamo mwaka 1982 alitunukiwa shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) kutoka chuo hicho hicho cha Lateran (Roma). Hiki ni kitabu chake cha tisa katika mfululizo wa machapisho yake. Tarehe 4 Februari 2008, Jaji Bwana aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania. Kabla ya hapo amekuwa Jaji kwa miaka kadhaa hapa Tanzania na nchini Seychelles.

Binding

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Haki, Amani na Maendeleo”

Your email address will not be published. Required fields are marked *