Mkuki Na Nyota Publishers

Haile Ngoma ya Wana: Diwani ya Mwanamvita

Author(s): Abdilatif Abdalla, Ahmad Nassir Juma Bhalo, Ahmed Hussein Ahmed, diwani, Kimvita, Mombasa, Muyaka wa Muhaji, Safal-Cornell

Sh 10,000

Diwani ya ushairi ya Kiswahili ya Ahmed Hussein Ahmed, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell, iliyoandikwa kwa lahaja ya Kimvita ya Mombasa. Inaweka Ahmed katika mfululizo wa Muyaka wa Muhaji, Ahmad Nassir Juma Bhalo, na Abdilatif Abdalla. Tathlitha, tarbia, na majibizano katika tungo zake.

Diwani ya ushairi ya Kiswahili iliyoandikwa kwa lahaja ya Kimvita (lahaja izungumzwayo jijini Mombasa) na Ahmed Hussein Ahmed, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell ya Fasihi ya Afrika. Lahaja ya Kimvita imetumiwa na washairi maarufu na wazoefu wa tungo katika nyakati mbalimbali kihistoria, kama vile Shaha Muyaka wa Muhaji, Ahmad Nassir Juma Bhalo, Abdilatif Abdalla, na sasa Ahmed Hussein Ahmed. Hii ni lahaja yenye manyumbulifu anuwai kwa namna sauti zake zinavyoleta maana tofauti zinapotamkwa, na ina ukwasi wa misamiati. Mashairi yaliyomo katika diwani hii yanaangazia mada mbalimbali zikiwemo utamaduni wa mwandishi, masuala ya maisha, mijadala ya kielimu, maswali na majibu, taanasi, na masuala ya kisasa. Vilevile mshairi ametumia mbinu mbalimbali za tasnifu ya tungo, kwa mfano tathlitha, tarbia, na majibizano kufikisha ujumbe wake. Diwani inaweka Kimvita katika mfululizo wa kihistoria wa fasihi ya Pwani.

Dimensions 195 × 130 mm
Binding

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Haile Ngoma ya Wana: Diwani ya Mwanamvita”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also like…