Diwani hii imeibua dhana moja kuu ambayo pia ni mhimili wa jina la kitabu hiki. Dhana hiyo ni binadamu na mtu. Mbali na ukweli kua mtu na binadamu ni majina mawili tofauti ambayo yanarejelea kiumbe kimoja, katika diwani hii inaonekana ni viumbe viwili tofauti ila vyenye nasaba moja. Binadamu akiwa amebeba dhana ya mzoga na mtu mumo humo, utu ukiwa amebeba dhana ya kunukia.
Kwa maana nyingine, binadamu ni yule kiumbe razini mwenye chembechembe za uhayawani ndani yake, ilhali mtu ni kiumbe razini aliye katika ukamilifu wa urazini kwa matendo pendeka katika jamii ya warazini. Hivyo, dhana hiyo inaibua maovu (mzoga au matendo yafanywayo na binadamu) na mema (chakula kinachonukia au matendo yafanywayo na mtu). Kwa mantiki hiyo, mzoga ni binadamu waovu na vitendo viovu vyote, ilhali chakula ni watu wema na matendo mema yanayomfaa kila kiumbe hai.
Kuhusu Mwandishi
Lenard Mtesigwa ni mwandishi wa tamthiliya, riwaya na hadithi fupi za Kiswahili. Alianza kazi ya utunzi kati ya Machi hadi Mei 2015, akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala cha nchini Tanzania.
Kazi yake ya kwanza ilikuwa ni tamthiliya iliyotungwa kwa lengo la kutumika katika somo la Kiswahili. Kazi zilizofuata zilikua ni riwaya pamoja na ushairi kwa lengo la kutumika katika kozi husika ya Kiswahili.
Reviews
There are no reviews yet.