Kitabu cha pili katika mfululizo wa Uwazi na Ukweli vyenye hotuba za kila mwisho wa mwezi za Rais Benjamin W. Mkapa. Katika kitabu hiki, Mkapa anazungumzia matukio mema na mabaya ya mwaka 2002, pamoja na hatua za maendeleo zilizopigwa na taifa katika nyanja za kisiasa, kijamii, na kiuchumi. Rais Mkapa anaeleza kwa kina maana na athari za utandawazi kwetu kama taifa na kwa watu binafsi. Anaendelea kueleza, kufafanua, na kutetea sera ya ubinafsishaji na kuonyesha matunda ya sera hiyo bila kupuuza sokomoko kama ile iliyofuatia hatua ya kubinafsisha shirika la TANESCO. Pia anaelezea masuala ya siasa, hasa utekelezaji mzuri wa MWAFAKA kati ya CCM na CUF kule Zanzibar, ulioashiria utulivu wa kisiasa nchini na kurejesha upendo na mshikamano wa wananchi Visiwani. Kwa viongozi, walimu, na wanafunzi wa ngazi zote.

Uwazi na Ukweli – 2
Author(s): 2002, Awamu ya Tatu, Benjamin W. Mkapa, hotuba, Kiswahili, MWAFAKA, ubinafsishaji, utandawazi, Uwazi na Ukweli
Sh 7,000
Kitabu cha pili katika mfululizo wa Uwazi na Ukweli cha hotuba za Rais Benjamin W. Mkapa. Inazungumzia matukio ya mwaka 2002: utandawazi, ubinafsishaji (pamoja na TANESCO), na MWAFAKA kati ya CCM na CUF Zanzibar. Kwa viongozi, walimu, na wanafunzi wa ngazi zote.
| Weight | 0.6 kg |
|---|---|
| Dimensions | 203 × 127 mm |
| Binding |




Reviews
There are no reviews yet.