Kumbukumbu za Peter D. M. Bwimbo, aliyekuwa Mlinzi Mkuu wa Rais Julius Nyerere na Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi wa Viongozi. Tarehe 20 Januari 1964, maofisa 15 wa Jeshi la Tanganyika walioongoza maasi ya kijeshi dhidi ya serikali, na kikundi kimoja kilikwenda Ikulu kutaka kumlazimisha Rais Nyerere kukubali matakwa yao. Kwa ujasiri na ubunifu, Bwimbo aliwahamisha Rais Nyerere na Makamo wake Rashid Kawawa, akawapeleka mahali salama. Operesheni hii ikaitwa Operesheni Magogoni. Katika kitabu hiki, Bwimbo anatoa siri ambayo ni wachache sana waliyoifahamu, pamoja na historia ya Kitengo cha Ulinzi wa Viongozi katika Idara ya Usalama wa Taifa. Bwimbo alipewa Nishani ya Ushupavu (Gallantry Medal) mwaka 1985 kwa ujasiri wake wakati wa Operesheni Magogoni.

Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere
Author(s): 1964 Army Mutiny, Julius Nyerere, Kiswahili, Operesheni Magogoni, Peter D.M. Bwimbo, Rashid Kawawa, Tanzania, usalama wa taifa
Sh 15,000
Kumbukumbu za Kiswahili za Peter D. M. Bwimbo, Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere wakati wa maasi ya jeshi ya Januari 1964. Maelezo ya siri ya Operesheni Magogoni iliyomuokoa Rais Nyerere na Makamo wake Rashid Kawawa. Pia historia ya Kitengo cha Ulinzi wa Viongozi katika Idara ya Usalama wa Taifa.




Reviews
There are no reviews yet.