Diwani ya ushairi ya Kiswahili iliyoandikwa na Rashid Othman Ali, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell. Mji wa Kambare ni diwani iliyotungwa kwa umahiri na ustadi wa aina yake, kuweza kumvutia kila msomaji, awe ni mwanafasihi, mwanaisimu, au mtu wa fani yoyote. Inatokana na uteuzi mzuri wa misamiati inayolandana vina na mizani kiasi ya kuukonga moyo wa msomaji. Muwala, ufundi mkubwa katika kupangilia maneno, ujenzi wa taswira na lugha ya picha, ubobezi katika kumfikirisha msomaji, upana wa dhamira na maudhui yanayopatikana katika tungo zilizomo zinagusia takriban nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Diwani imetumia kwa kiasi kikubwa lahaja za kizanzibari, hasa kipemba. Pia kuna maneno ya Kiswahili asilia yanayoongeza vionjo vya lugha na utamu wa michapo ya mashairi na tungo za Kiswahili cha uswahilini. Maneno magumu yamefafanuliwa maana mwishoni. Itawafaa wapenzi wa mashairi, walimu, wakufunzi, na vikundi vya tamaduni na sanaa.

Mji Wa kambare
Author(s): diwani, Kiswahili, lahaja ya kipemba, lugha ya picha, Rashid Othman Ali, Safal-Cornell, ushairi, Zanzibar
Sh 15,000
Diwani ya ushairi ya Kiswahili ya Rashid Othman Ali, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell, iliyoandikwa kwa lahaja ya kipemba. Inalenga wapenzi wa mashairi, wanaisimu, walimu, wakufunzi, na vikundi vya sanaa. Maneno magumu yamefafanuliwa mwishoni.
ISBN: 9789987082247
Category: Poetry
Tags: diwani, Kiswahili, lahaja ya kipemba, lugha ya picha, Rashid Othman Ali, Safal-Cornell, ushairi, Zanzibar
| Dimensions | 195 × 130 mm |
|---|---|
| Binding |
Be the first to review “Mji Wa kambare”Cancel Reply
You may also like…
Related products
-

N’na Kwetu
Sh 15,000 -

Mungu Hakopeshwi
Sh 20,000 -

Chemichemi Jangwani
Sh 12,000 -

Haile Ngoma ya Wana: Diwani ya Mwanamvita
Sh 10,000

Reviews
There are no reviews yet.