Mchezo wa kumi na tisa katika mfululizo wa vitabu vya michezo ya kuigiza kutoka Tanzania Publishing House. Michezo hii imeendelea kuburudisha na kuelimisha wasomaji wa rika zote tangu ilipochapishwa kwa mara ya kwanza, na imechaguliwa kufundishia lugha na drama mashuleni. Kilio Chetu ni tamthilia inayovunja ukimya uliotawala miongoni mwa jamii katika kutatua matatizo makubwa ambayo chimbuko lake ni mahusiano ya kijinsia. Katika tamthilia hii, vijana wanatoa sauti ya jitimai iliyojaa sononeko na shutuma dhidi ya wazazi, walezi, na viongozi ambao wanafumbia macho suala hili nyeti. Ndiyo maana tamthilia hii inasisitiza sana haja ya kuwapa vijana elimu juu ya mahusiano ya kijinsia badala ya hofu na vitisho ambavyo vimedhihirika kupitia hali halisi kuwa vimeshindwa.

Kilio Chetu
Author(s): Kiswahili, mahusiano ya kijinsia, mchezo wa kuigiza, Medical Aid Foundation, shule, tamthilia, Tanzania Publishing House, vijana
Sh 6,000
Tamthilia ya Kiswahili kutoka Medical Aid Foundation, mchezo wa kumi na tisa katika mfululizo wa Tanzania Publishing House. Inavunja ukimya kuhusu mahusiano ya kijinsia kati ya vijana, na kusisitiza umuhimu wa elimu badala ya hofu na vitisho. Imechaguliwa kufundishia lugha na drama mashuleni Tanzania.




Reviews
There are no reviews yet.