Kanga ni nguo ya jadi inayovaliwa na baadhi ya wanawake wa Afrika Mashariki.
Je, umewahi kujiuliza ni njia ngapi zipo za kutumia kanga? Usijiulize zaidi! Tumbukia kwenye hadithi hii inayosimuliwa na mtoto juu ya kanga ya Mamaye, na jinsi kanga hiyo inavyofungua wezekano zisizo na mwisho ujipatie majibu!
Maria G. N. Biswalo | Mwandishi
Kama mwalimu wa kimataifa na mama wa watoto wa tamaduni mbili, Maria G. N. Biswalo alibaini ukosefu wa uwakilishi katika maandishi ya hadithi za watoto wadogo, zionyeshazo tamaduni yake ya Kitanzania na lugha mama- Kiswahili. Kupitia hadithi zake, Maria ana matamanio ya kuziba pengo hili kwa kuibua na kuhamasisha upatikanaji rahisi wa hadithi nyingi za watoto za Kitanzania duniani kote. Anakualika kuungana naye kupitia tovuti ya www.hadithizamama.com.
Theresia Mmasi | Usanifu wa Picha
Theresia Mmasi ni mtengenezaji wa taaluma anuwai wa Kitanzania na anayependa michoro, historia na elimu ya sanaa. Yeye si tu ana fikra bunifu, bali pia muundaji na mtendaji. Theresia anajishughulisha na miradi inayotumia sanaa ya picha kama zana ya kuunda ulimwengu jumuishi zaidi, endelevu, na wa haki. Anaaminikuwa ufundi wa picha ni zana wazi inayowezesha jamii zenye changamoto kumiliki na kusimulia hadithi zao.





Reviews
There are no reviews yet.