Kitabu cha kwanza chenye historia ya kina ya Simba Sports Club, moja ya klabu maarufu zaidi za soka nchini Tanzania. Kwa mpenzi wa soka na hasa mkereketwa wa Simba, utajua chimbuko na undani wake tangu ilipoanzishwa hadi hii leo. Vilevile utaweza kukitumia kama ushahidi katika mabishano na mijadala. Utasoma vioja vya soka letu: ushabiki wa kupindukia, vituko, imani za kishirikina, makundi yaliyotia fora, migogoro, mafanikio, picha za matukio mbalimbali, na rekodi za mwenendo wa timu. Utafahamu pia ni lini soka liliingia Tanzania, mpasuko uliozaa Simba na Yanga, na mengine mengi. Mwandishi Mwina Kaduguda amefanya utafiti wa kina kutoka vyanzo vya rasmi (maktaba, vitabu, magazeti na mahojiano na wazee), na kuzalisha rekodi zisizopatikana kwa urahisi.

Historia ya Klabu ya Simba
Author(s): African football, Dar es Salaam, historia ya soka, Mwina Kaduguda, Simba Sports Club, soka la Tanzania, sports history, Yanga rivalry
Sh 7,000
Historia ya kina ya Simba Sports Club tangu kuanzishwa hadi hii leo: vioja, ushabiki wa kupindukia, imani za kishirikina, migogoro, mafanikio, picha za matukio, na rekodi za mwenendo wa timu. Pia mpasuko uliozaa Simba na Yanga. Kitabu cha kwanza cha aina yake cha Mwina Kaduguda, kwa wapenzi wa soka la Tanzania.
| Weight | 0.6 kg |
|---|---|
| Dimensions | 270 × 175 mm |
| Binding | |
| Pages |




Reviews
There are no reviews yet.