Riwaya classic ya Kiswahili ya Ben Mtobwa, kitabu chake cha mwisho. Akiwa bado kijana mdogo, Mtukwao anatoroshwa kijijini na familia yake ili aokoe uhai wake ulio katika hatihati ya kupotelea mikononi mwa wanakijiji. Safari inamjia ghafla kama jinamizi na kumfungulia dunia mpya yenye chungu na tamu, lakini chungu ni zaidi. Ni pale anapokumbuka kitu muhimu sana alichokipoteza wakati wa pilika zake za maisha, ndipo anapopata wazo la kurudi kwao ili akatengeneze mambo yake. Lakini imekwishapita miaka zaidi ya thelathini tangu aondoke kijijini. Je, familia yake, ambayo ndiyo ina dhamana pekee ya kumsaidia, bado ipo? Ama ndiyo ng’ombe wa maskini hazai? Katika kitabu hiki cha mwisho, Ben Mtobwa anathibitisha tena uwezo wake mkubwa wa kutumia kalamu yake bila kubahatisha. Kinachotofautisha riwaya hii na riwaya nyingine zake ni namna alivyohama kabisa kutoka kwenye maudhui ya kijasusi na kuchambua uhalisia wa Watanzania wengi.

Kiguu Na Njia
Author(s): Ben Mtobwa, classic, Kiswahili, Mtukwao, riwaya, safari, Tanzania, urithi
Sh 15,000
Riwaya ya mwisho ya Ben Mtobwa. Mtukwao anatoroshwa kijijini akiwa mtoto, anatembea karibu kila mkoa wa Tanzania, na baada ya miaka thelathini anarudi kutafuta familia yake. Ben Mtobwa anahama kutoka maudhui ya kijasusi kwenda uchambuzi wa uhalisia wa Watanzania wengi. RIGHTS-CANDIDATE.
| Weight | 0.7 kg |
|---|




Reviews
There are no reviews yet.