Mkuki Na Nyota Publishers

Vitimbi vya Mama wa Kambo na Hadithi Nyingine

Author(s): Ally Yusuf Mugenzi, BBC Idhaa ya Kiswahili, hadithi fupifupi, Idhaa ya Maziwa Makuu, Kiswahili, mauaji ya kimbari, Radio Rwanda, uandishi wa habari

Sh 15,000

Mkusanyiko wa hadithi fupifupi za Kiswahili za Ally Yusuf Mugenzi, mtangazaji wa zamani wa Redio Rwanda na mhariri wa BBC Idhaa ya Maziwa Makuu. Hadithi kutoka kipindi cha Hadithi na Muziki cha Redio Rwanda ya miaka ya 1980 na 1990, zinazotumiwa katika mitaala ya shule.

Mkusanyiko wa hadithi fupifupi za Kiswahili zilizoandikwa na Ally Yusuf Mugenzi. Vitimbi vya Mama wa Kambo, Wivu, Radhi za Wazazi, Rafiki Maluuni, Mchumba Kaka, na Adui Mama ni hadithi zinazosawiri jamii alimochipukia mwandishi, au kuishi na kufanya kazi akiwa polisi, mwandishi wa habari, na mtangazaji wa redio katika nchi za Tanzania, Rwanda, Burundi, na Uingereza kwa takribani miaka 40. Kitabu hiki ni matokeo ya maombi ya watu wengi waliomsikiliza katika kipindi cha Hadithi na Muziki cha Redio Rwanda katika miaka ya 1980 na 1990. Hadithi hizi pia zimekuwa zikitumiwa na wakuza mitaala mashuleni. Mugenzi alijiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari Tanzania mwaka 1978, aliajiriwa na SHIHATA, alihamia Redio Rwanda, kisha BBC, ambapo alianzisha idhaa ya kukutanisha watu waliotenganishwa na mauaji ya kimbari ya Rwanda, baadaye ikaitwa Idhaa ya Maziwa Makuu, anayoiongoza hadi sasa.

Weight 0.4 kg
Dimensions 195 × 130 mm
Binding

Pages

Year published

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Vitimbi vya Mama wa Kambo na Hadithi Nyingine”

Your email address will not be published. Required fields are marked *