Kitabu cha Kiswahili cha msaada binafsi kilichoandikwa na S. L. Makonga. Mawazo yana nafasi kubwa sana katika maisha ya binadamu; yanaweza kumjenga vyema mtu au kumharibia maisha yake yote. Mara nyingi tunajiwekea mawazo vichwani mwetu ambayo hutufanya tujione wadhaifu na duni, lakini mawazo hayo si sahihi, na kama tu tukipata tiba iliyotabibu twaweza kuyashinda mawazo hayo potofu. Tiba ya Ugonjwa wa Mawazo ni kitabu kinachokufunza kuhusu mawazo potofu na kukuonesha athari zake, lakini pia kukupa suluhisho la mawazo haya yasiyojenga na yanayoweza kusababisha madhara makubwa katika maisha yetu. Kwa makusudi kabisa, mwandishi amezitumia methali tuzitumiazo kila siku kama vichwa vya insha, ili kuonesha jinsi methali hizo zinavyohusiana na mawazo yetu na zinavyoweza kuwa chachu ya tiba ya mawazo potofu. Kusudio la kitabu ni kuwasaidia watu wa rika mbalimbali na jinsia zote, wasomi na wasio wasomi.

Tiba ya Ugonjwa wa Mawazo – 1
Author(s): Kiswahili, kitabu cha msaada, maendeleo binafsi, mawazo, methali, mtu chanya, S. L. Makonga, saikolojia
Sh 10,000
Kitabu cha Kiswahili cha msaada binafsi cha S. L. Makonga. Mawazo potofu, athari zake, na njia za kuyashinda. Mwandishi anatumia methali za kila siku kama vichwa vya insha kuonyesha uhusiano kati ya methali na saikolojia ya kujenga mtu chanya. Kwa wasomaji wa rika zote.
| Dimensions | 230 × 150 mm |
|---|---|
| Binding | |
| Pages |




Reviews
There are no reviews yet.