Tamthilia ya Kiswahili ya Amandina Lihamba, iliyotohotiwa kutoka riwaya ya The Money Order (Le Mandat) ya mwandishi mashuhuri wa Senegali, Sembene Ousmane. Tamthilia hii inajadili mfumo wa urasimu uliorithiwa na nchi nyingi za Afrika kutoka kwa wakoloni na athari zake kwa jamii. Ibrahim Chande anafurahi sana anapopokea hawala ya shilingi 2,000 kutoka kwa mpwaye aliyeko masomoni Landani. Lakini hawezi kuzuia habari hizo nzuri kuwafikia majirani na wenye maduka mtaani. Wote wanamzengea wakitazamia chochote kutokana na fedha hizo, licha ya kwamba fedha si zake. Hata hivyo, matatizo ya urasimu yanajiingiza kati yake na hawala. Inasambazwa kimataifa na African Books Collective.
Swahili play adapted from Sembene Ousmane’s The Money Order.





Reviews
There are no reviews yet.