Mkuki Na Nyota Publishers

Wasifu wa Siti Binti Saad

Sh 6,000

Shaaban Robert

Kwa zaidi ya miaka kumi na tano vitabu vya mwandishi na mshairi maarufu kushinda wote katika jamii za Waswahili kote Afrika ya Mashariki na kati, Marehemu Sheikh Shaaban Robert, havikupatikana Tanzania.

Sababu ya kukosekana kwa vitabu hivyo ni kuwa kampuni ya kigeni iliyovichapisha iliamua kuacha kuvichapisha kwa sababu haikulipwa kwa fedha za kigeni jambo lililosababishwa na hali mbaya ya uchumi.

Athari za kupotea kwa vitabu vya sheikh Shabaan Robert katika miaka hiyo ni kwamba Watanzania wengi hasa wale wenye umri wa chini ya miaka thelathini, hawamjui mwandishi huyu maarufu na hawakulelewa katika mazingira ya utajiri wa maandishi yake ambayo bila shaka yoyote ni mfano pekee wa utajiri wa urithi wa utamaduni watu.

Kwa kuvichapisha vitabu vya Marehemu Sheikh Shaaban Robert, tunawakaribisha tena Watanzania, hasa vijana, kuvisoma, kuburudishwa na kufunzwa na yale aliyoyaandika kwa sanaa na kipaji adimu

Dimensions 205 × 147 mm
Binding

Pages

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Wasifu wa Siti Binti Saad”

Your email address will not be published. Required fields are marked *