Mkuki Na Nyota Publishers

Dhulma

Author(s): Abdulrazak Gurnah, Badar, Dar es Salaam, Ida Hadjivayanis, Karim, Nobel Prize, tafsiri, Zanzibar

Sh 40,000

Tafsiri ya Kiswahili ya Theft, riwaya ya hivi karibuni ya Abdulrazak Gurnah, iliyofanywa na Dkt. Ida Hadjivayanis. Tafsiri ya pili ya Gurnah katika Kiswahili (baada ya Peponi, Row 302) na ya kwanza tangu Tuzo ya Nobel ya 2021. Vijana watatu, Badar, Karim, na Fauzia, wanapita safari ya mapenzi, kazi, na hatimaye usaliti katika Zanzibar na Dar es Salaam.

Tafsiri ya Kiswahili ya Theft, riwaya ya hivi karibuni ya Abdulrazak Gurnah, mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi ya mwaka 2021. Hii ni tafsiri ya pili ya riwaya za Gurnah katika Kiswahili, ikitanguliwa na Peponi (Row 302). Mtafsiri ni Dkt. Ida Hadjivayanis, Mhadhiri Mwandamizi wa Masomo ya Kiswahili SOAS, Chuo Kikuu cha London. Katika mitaa ya Zanzibar na Dar es Salaam, maisha ya vijana watatu, Badar, Karim, na Fauzia, yanasukwa na matukio yasiyotabirika. Badar, kijana maskini asiye na mizizi wala elimu, anajikuta katika dunia ya watu wenye mamlaka na mali. Akiwa mtumishi, anakutana na Karim, kijana wa mama mwenye nyumba mwenye ndoto na matarajio makubwa. Wakati huo Fauzia, akielemewa na changamoto za utotoni, anatafuta njia ya kujinasua. Vijana hawa wenye njozi tofauti lakini mustakabali uliofungamana wanapita kwenye safari ya mapenzi, kazi, na uzazi, huku urafiki wao ukijaribiwa na tamaa, hofu, mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia, na hatimaye usaliti. Hii ni tafsiri ya kwanza ya riwaya ya Gurnah baada ya kupokea Tuzo ya Nobel.

Weight 0.4 kg

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Dhulma”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also like…