Riwaya ya kusisimua ya kijasusi ya Kiswahili iliyoandikwa na Enock Maregesi, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell. Hii ni riwaya ya kusisimua ya kijasusi na madawa ya kulevya, inayozungumzia vita kati ya Tume ya Dunia ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya na Ugaidi wa Kimataifa (World Drugs Enforcement Commission, WODEC) na shirika kubwa la madawa ya kulevya la Kolonia Santita (CS-14) la Kolombia na Meksiko. Riwaya inaelezea kwa kinagaubaga jitihada za pamoja kati ya Tume ya Dunia, Marekani, na Meksiko za kuwasaka na hatimaye kuwatia nguvuni viongozi nduli wa CS-14, na kuzuia shehena kubwa ya madawa ya kulevya na malighafi ya nyukilia kwenda Afrika, Asia, Amerika, na Ulaya. Ukisoma kitabu hiki utajiuliza jinsi mwandishi alivyoweza kusuka riwaya inayoufanya moyo kuenda mbio. Enock Maregesi ni gwiji wa uandishi wa riwaya za kijasusi, na Kolonia Santita imeweka kiwango kipya cha juu kitakachowaumiza vichwa waandishi wengine.

Kolonia Santita: Laana ya Panthera Tigrisi
Author(s): Enock Maregesi, Kiswahili, Kolombia, madawa ya kulevya, Meksiko, riwaya, Safal-Cornell, WODEC
Sh 30,000
Riwaya ya kusisimua ya kijasusi ya Enock Maregesi, mshindi wa Tuzo ya Safal-Cornell. Vita kati ya Tume ya Dunia ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya na shirika la Kolonia Santita la Kolombia na Meksiko. Shehena za madawa na malighafi ya nyukilia, operesheni za kimataifa. RIGHTS-CANDIDATE.
| Dimensions | 195 × 130 mm |
|---|---|
| Binding |
You may also like…
-

The African Epic Controversy
Sh 45,000




Reviews
There are no reviews yet.