Mkuki Na Nyota Publishers

Uhuru wa Mahakama

Author(s): Bangalore Principles, Barnabas A. Samatta, Jaji Mkuu, Kiswahili, Mzumbe, rushwa, uhuru wa mahakama, usawa wa sheria

Sh 35,000

Kitabu cha sheria cha Jaji Barnabas A. Samatta, Jaji Mkuu wa Tanzania (2000-2007) na mjumbe mwanzilishi wa Judicial Integrity Group. Inazungumzia uhuru wa mahakama, rushwa, ugumu wa kazi ya jaji, mikwaruzano kati ya mihimili ya dola, na mamlaka ya kiuonevu. Kwa mwanasheria na mlei, mtawala na mtawaliwa.

Kitabu cha sheria kwa Kiswahili kilichoandikwa na Jaji Barnabas A. Samatta, aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania kutoka 2000 hadi 2007. Kabla ya hapo, 1984-1987, alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zimbabwe. Ni mjumbe mwanzilishi wa Judicial Integrity Group, chombo huru cha kimataifa kinachojishughulisha na ukuzaji wa uadilifu wa mahakama duniani, chombo kilichotunga Kanuni za Bangalore za Mwenendo wa Mahakama. Jaji Samatta ni Mwenyekiti Mwenza wa Bodi ya Kampuni ya Earth, Energy and Environment Mediation Limited yenye makao London, inayoshughulikia njia bora za kutatua migogoro barani Afrika inayohusiana na ardhi, mafuta, madini, maji, na mazingira. Pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe. Katika kitabu hiki anazungumzia uhuru wa mahakama; rushwa; ugumu wa kazi na maisha ya jaji; mikwaruzano baina ya mihimili ya dola; na utumiaji wa kiuonevu wa mamlaka ya dola. Ni kitabu kwa mwanasheria na kwa mlei; kwa mtawala na mtawaliwa; kwa kila mtu.

Weight 0.6 kg
Binding

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Uhuru wa Mahakama”

Your email address will not be published. Required fields are marked *